Tuesday, 22 September 2015

ben carson achafua hali ya hewa marekani, muislamu hawezi kuongoza marekani



Mmoja wa wanasiasa wanaowania kuchaguliwa kugombea urais kwa niaba ya chama cha Republican, nchini Marekani amesema Uislamu hauambatani na katiba ya taifa hilo.

Ben carson  amezaliwa tarehe 18/09/1951 ni jina lenye mvuto na kutamkika na watu wengi zaidi duni ani kwa sasa
Dr. ben carson kwa sasa ametajwa kushiriki katika kinyang’anyiro cha kugombea uraisi wa marekani ila mwana harakati huyu alisema maneno ambayo watu wa dhehebu lingine wameshindwa kumuelewa
Mgombea huyu wa chama cha republican amesema hatomsapoti mgombea yeyote ambaye ana dini ya kiislamu
Amesema muislamu hafai kuwa raisi wa marekani kwasabau tu wanakinzana na katiba ya marekani
Ben Carson, ambaye ni, daktari wa neva aliyestaafu, amesema yeye katu hawezi kukubali Mwislamu kuwa rais wa Marekani.
Akijibu maswali katika kipindi cha mahojiano cha runinga ya NBC ''Meet the Press, Carson anasema kuwa dini hiyo inakinzana na katiba ya Marekani.
Kura ya maoni inaonesha kuwa daktari huyo ambaye ni mkristo anashikilia nafasi ya pili kwa umaarufu nyuma ya bilionea mbishi Donald Trump

Matamshi yake yanatokea siku chache, baada ya mgombea anayepigiwa upatu kutwaa tikiti ya chama cha Republican, Donald Trump, kukataa kujitenga na mfuasi wake, ambaye alimshutumu Rais Obama kuwa Mwislamu, na hata sio Mmarekani.

Source BBC swahili

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...