Monday, 21 September 2015

mama samia suluhu mkoani tanga

Monday, September 21, 2015

mama samia akiwa Tanga maelfu ya wakazi wa Tanga wahudhuria

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Mama Samia Suluhu Hassan, akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Uwanja wa  Usagara jimbo la Tanga, leo

Wananchi wakimshangilia Mgombea Mwenza wa Urais Mama Samia Suluhu Hassan lipohutubia mkutanowa kampeni katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Uwanja wa Usagara jimbo la Tanga, leo
 Mgombea Ubunge jimbo la Bumbuli, January Makamba, akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika Uwanja wa Usagara jimbo la Tanaga, leo
 Aliyekuwa muwania Ubunge jimbo la Nkenge Asupta Mshama lakini hakupita katika kura za maoni za CCM, akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika viwanja vya Usagara jimbo la Tanga, leo.









Naibu  Waziri wa Sheria na Katiba, Ummy Mwalimu, akihutubia mkutano wa kampeni uliofayika leo katika Viwanja vya Usagara jimbo la Tanga.

Mgobea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akifurahia jambo na Mgombea Ubunge jimbo la Tanga, Omari Nundu wakati wa mkutano wakampeni uliofanyika leo katika jimbo hilo.
 Mgombea Ubunge jimbo la Bumbuli, Januari Makamba akiteta jambo na Naibu Waziri wa Sheria na Katiba, Ummy Mwalimi katika mkutano wa kampeni uliofayika leo katika Viwanja vya Usagara nje kidogo ya jiji la Tanga
Mratibu wa Mama Sema na Mwanao, Steven Mengere maarufu wa jina la Steve Nyerere, akifurahia jambo la Msanii wa Bongo Movie, Wema Sepetu wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Usagara jimbo la Tanga, leo
 Wananchi wakiwa wamefurika barabarani kuzuia msafara wa mgombea Mweza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu hasani katika akienda kuhutubia mkutano wa kampeni kwenye viwanja vya Usagara nje kidogo ya jiji la Tanga, leo
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Muheza mkoa wa Tanga
 Mgombea Ubunge jimbo la Muheza, Adadi Rajab akiomba kura baada ya kunadiwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan (kulia) katika mkutano wa kampeni uliofayika katika jimbo hilo leo
Wananchi wakimshangilia Mgobea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipohutubia mkutano wa kampeni leo katika jimbo la Muheza mkoa wa Tanga
 Wananchi wakiwa wamezuia msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika eneo la Kigombe, Muheza mkoani Tanga leo
 Baadhi ya viongozi wa CCM wakiwa katika Kivuko cha Mv Pangani wakati msafara wa mgombea Mwenza wa Urais Mama Samia Suluhu Hassan ukienda jimbo la Bweni, katika jimbo la Pangani mkoa wa Tanga kuhutubia mkutano wa kampeni. Kuslia ni Ofisa Mwandamizi kutoka Makao Makuu ya CCM, Mama Chitinka.
 Kina mama wakikimbia kuwahi kumlaki Mgombea Mwenza wa CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili Bweni kuhutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Pangani mkoani Tanga leo
 Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Pangani, Mama  Regina Sonjo akihutubia mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika leo, katika eneo la Bweni jimbo la Pangani mkoani Tanga leo.

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...