Tuesday, 12 September 2017

Jay dee Arudi tena

Ni muda mrefu mashabiki wametamani kumsikia tena Lady Jaydee baada ya ukimya wake wa takribani miezi mitano.


Jay Dee Kuachia Ngoma Mpya Ijumaa
Hatimaye malkia huyo wa Bongo Flava, Jumanne hii ameachia wimbo wake mpya ‘I Miss You’ ambayo imetayarishwa na Man Walter. Lakini bado kiu ya mashabiki wanatamani kuiona video ya wimbo huo.

Akiongea na Bongo5, mmoja ya watu wa karibu wa msanii huyo amesema, video ya wimbo huo itatoka rasmi siku ya Ijumaa hii na imeongozwa na Justin Campos nchini Afrika Kusini.

Video ya mwisho ya Jide ilikuwa ni ‘Rosella’ aliyofanya na kundi la H_art The Band kutoka nchini Kenya ambapo pia wimbo huo unapatikana katika albamu yake mpya, Woman. Hizi ni baadhi ya picha zinazoweza kuonekana katika wimbo huo

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...