
Hayo yamewekwa wazi na taarifa iliyotolewa na ukurasa maalum wa Simba SC usiku wa kuamkia leo baada ya timu yao kutoka sare ya bila kufunguna na wapinzani wao wa siku hiyo Azam FC ambapo kila mmoja alitamani kumfunga mwenzake ili aweze kujiwekea rekodi mpya lakini kwa bahati mbaya mambo yakaenda ndivyo sivyo.
"Kiungo mahiri wa Simba, James Kotei amechaguliwa na wapenzi wa Simba kuwa mchezaji bora wa mechi dhidi ya Azam FC", imesema taarifa hiyo.
James Kotei amesaini kandarasi ya miaka miwili ya kuwatumikia wekundu wa Msimbazi, Simba SC baada ya kumalizika mkataba wake wa awali aliokuwa akiutumikia hapo msimbazi wa miezi sita
No comments:
Post a Comment