Monday, 23 October 2017

klopp ajitoa kwenye mbio za ubingwa ligi kuu uingereza

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema mbio za kuwania ubingwa wa ligi kuu ya soka nchini England EPL ni kama zimefika mwisho kutokana na mwendelezo mzuri wa Manchester City.
Akiongea kuelekea mchezo  wa EPL kati ya timu yake ya Liverpool dhidi ya Tottenham Klopp amekiri hilo kwa kudai haoni nafasi kwa timu zingine kwasababu Manchester City haioneshi dalili za kukwama.
“Manchester City inafanya vizuri na nafikiri wananafasi kubwa zaidi ya kutwaa ubingwa kuliko timu zingine japokuwa kwenye soka lolote linawezekana amesema”, amesema Klopp
Liverpool ambayo ina pointi 13 katika nafasi ya 8 imekuwa haina mwendelezo mzuri kwenye ligi japokuwa Klopp ana imani na timu yake kuwa inaweza kufanya vizuri.
Endapo Liverpool itashinda leo dhidi ya Tottenham itafikisha alama 18 na kupunguza tofauti ya alama dhidi ya vinara Manchester City wenye alama 25

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...