Friday, 1 December 2017

faida na hasara ya mazoezi wakati umechoka

 Kufanya mazoezi, baada ya pilika pilika nyingi za siku ambazo huifanya miili yetu kugubikwa na uchovu, yaweza kuonekana kwamba itatuongezea uchovu maradufu, lakini kufanya mazoezi kutasababisha miili yetu kuchangamka na kuondokana na uchovu.

Kufanya mazoezi kwa dakika 30 kutaboresha mzunguko wa damu mwilini ambapo kutapelekea kusambazwa kwa hewa ya Oksijeni ( Oxygen) na sukari (glucose) katika ogani mbali mbali za mwili, hususan katika ubongo. Hii
itatusaidia kuondokana na hali ya uchovu, kupunguza msongo wa mawazo na kuwa na utulivu.


Katika utafiti mmoja uliochapishwa na jarida la Madawa na sayansi ya michezo, " Kila tunachofanya hutumia gesi ya Oksijeni , kwa hiyo kufanya mazoezi huimarisha mifumo ya miili yetu na hutuongezea ufanisi katika ufanyaji kazi bila kuchoka kwa urahisi, pia huboresha uwezo wa ufanyaji kazi wa ubongo(kufikiri na kumbukumbu)"

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...