Friday, 1 December 2017

UNYONYESHAJI WA WATOTO NI MUHIMU KWA UCHUMI WA DUNIA(WHO,UNICEF)

UWEKEZAJI KATIKA UNYONYESHAJI WA WATOTO NI MUHIMU KWA UCHUMI WA DUNIA(WHO,UNICEF)
Mchanganuo mpya umeonyesha kuwa, uwekezaji wa kiasi cha dola 4.70 za kimarekani kwa kila mtoto anayezaliwa, utauingizia uchumi wa dunia takriban dola 300 bilioni za kimarekani ifikapo mwaka 2025.


GENEVA. Hakuna nchi yeyote duniani iliyoweza kufikia kwa utimilifu  viwango vya unyonyeshaji watoto ulimwenguni pote, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya  shirika la afya duniani WHO na shirika la watoto UNICEF
wakishirikiana na taasisi ya unyonyeshaji (Global breastfeeding collective)  katika mpango wa kuongeza viwango ya unyonyeshaji watoto ulimwenguni.

Taasisi hiyo ilifanya upembuzi yakinifu kwa nchi 194 na kugundua kuwa ni asilimia 40 pekee ya watoto walio chini ya miezi sita walionyonyeshwa bila kupewa chakula kingine na ni nchi 23 peekee zilizokuwa na zaidi ya asilimia 60 za viwango vya unyonyeshaji bila kuwapa chakula kingine watoto walio chini ya umri wa miezi sita.

Utafiti umeonyesha kuwa, unyonyeshaji wa watoto  unaboresha afya ya akili, na faida nyingine nyingi kiafya kwa wote mama na mtoto. Unyonyeshaji wa watoto chini ya miezi sita bila kuwapa chakula kingine  umesaidia kuwaepusha watoto na magonjwa hatari kama kuhara na homa ya mapafu ambayo ni magonjwa hatari yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya watoto. Kina mama wanaonyonyesha wamepunguza uwezekano wa kupata magonjwa kama saratani ya kizazi na matiti ambayo ni magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vya kina mama.

"Maziwa ya mama yanampa mtoto mwanzo mzuri wa maisha yake" Anasema Dr Tedros Adhanom mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO na anaendelea kusema kuwa, "Maziwa ya mama yanafanya kazi kama chanjo ya mwanzo kabisa ya mtoto, na huwalinda watoto wachanga dhidi ya magonjwa hatari pamoja na kuwapatia virutubisho muhimu ambavyo huimarisha afya zao".

Moja ya kisa cha uwekezaji katika unyonyeshaji kwa nchi zinazoibukia kiuchumi- China, Indonesia, India, Nigeria na Mexico- kushindwa kuwekeza katika unyonyeshaji kulisababisha vifo vya takriban watoto 236 000 kwa mwaka pamoja na upotevu wa dola 119 bilioni za kimarekani katika uchumi.


Uwekezaji wa unyonyeshaji ulimwenguni ni wa kiwango cha chini. Kila mwaka, serikali za nchi za kipato cha chini na cha kati, huwekeza takriban dola 250 milioni za kimarekani kuhamasisha unyonyeshaji wa watoto na wafadhili huchangia dola 85 milioni pekee 

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...