Tuesday, 22 September 2015

apple wavamiwa kitekinolojia nchini china

Kampuni iliyodaiwa kutengeneza simu bandia 41,000 aina ya Iphones kutoka kampuni ya Apple imevamiwa huko Uchina na watu 9 kukamatwa.
Oparesheni hiyo ilishirikisha mamia ya wafanyikazi waliokuwa wakiandaa vipuri vya simu vilivyotumika kama simu mpya aina ya iphone tayari kuuzwa nje,huku simu hizo bandia zikizalisha kitita cha dola miloni 19.
Kampuni hiyo iligunduliwa tarehe 14 mwezi Mei lakini ikabainika katika mitandao ya kijamii na ofisi ya usalama ya umma Beijing siku ya jummapili.
Oparesheni hiyo ilianzishwa mwezi wa januari.
Image result for apple phones
Uchunguzi huo uliongozwa na kundi la mke na mumewe kaskazini mwa mji mkuu wa Uchina, kulingana na mamlaka ya Beijing.
Walisema kuwa walidokezewa na mamlaka ya Marekani ambayo ilinasa simu hizo bandia .
Ripoti hiyo inajiri wakati kuna msako wa bidhaa bandia unaotekelezwa na Uchina huku mamlaka hiyo ikiyashinikza makampuni kuweka nembo za ubora wa biadha.
Uchina pia imekubali kufanya kazi na mamlaka ya Marekani kupunguza kuwepo kwa bidhaa bandia zinazotoka nchi hizo mbili.
Image result for apple phones

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...