Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejiment ya
Utumishi wa Umma nchini Tanzania Celina
Kombani amefariki dunia.
Waziri Kombani ambaye pia alikuwa ni mbunge
wa jimbo la Ulanga mashariki, amefariki jana
Septemba 24, wakati akipata matibabu nchini
India.
Alizaliwa Juni 19, 1959, na alikuwa mbunge
kupitia chama tawala CCM.
Majonzi makubwa lufuatia taarifa za msiba
amefariki dunia leo huko India alikokuwa
akipata matibabu ya saratani.
Tayari mamlaka husika ikiwemo Serikali na
Bunge kupitia ofisi za Bunge zimethibitisha
kifo hicho na kubainisha kuwa, mwili wa
marehemu unategemewa kuwasili Tanzania,
siku ya Jumatatu, na shughuli zote Bunge na
Serikali zitasimamia maandalizi yote ya maziko
na kumsafirisha kwa mazishi nyumbani kwa
marehemu huko Mahenge.
Kabla ya kupatwa na umauti, marehemu alikuwa
Mbunge wa jimbo la Ulanga Mashariki na pia
alikuwa akigombea ubunge katika jimbo hilo
kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Friday, 25 September 2015
Waziri celina kombani afariki dunia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Featured Post
Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah
Mchezaji wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...
-
MAISHA ni vita bwana. Ili uweze kushinda, lazima upambane kweli. Wapo wanaoamini kuwa ‘kutusua’ kimaisha lazima uwe umesoma lakini huen...
-
KWA NINI WATOTO HUPOTEZA HAMU YA KULA? Kukosa hamu ya kula ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo hupelekea wazazi wengi kuwa na wasiwasi...
-
Mao alikuwa kiongozi Kichina Kikomunisti na mwanzilishi wa Jamhuri ya Watu wa China. Yeye alikuwa kuwajibika kwa sera za maafa ya ...
No comments:
Post a Comment