
Mshambuliaji wa Argentina Carlos
Tevez ameambiwa na mkufunzi mpya wa klabu yake ya Shanghai Shenhua
nchini China Wu Jingui kwamba ni mnene na hatachezea timu hiyo hadi
apunguze uzani na kuwa sawa kucheza.
Tevez, 33, ambaye anaaminika
kuwa miongoni mwa wachezaji wanaolipwa pesa nyingi zaidi duniani,
amefunga mabao mawili pekee katika mechi 12 tangu alipoanza kuwachezea
mwezi Machi.Wu, aliyechukua usukani katika klabu hiyo baada ya Gus Poyet kujiuzulu Jumatatu, pia alimkosoa kiungo wa kati qFredy Guarin.
"Ninafaa kuwajibika kwa timu na kwa wachezaji," alisema Wu.
"Wote wawili (Tevez na Guarin) wana uzani uliozidi kiwango. unapokuwa uwanjani, ikiwa huwezi kucheza 100%, basi haina maana."
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United na Manchester City alihamia Shanghai kutoka Boca Juniors.
Hata hivyo alikosa karibu nusu ya mechi za klabu hiyo msimu huu kutokana na majeraha.
No comments:
Post a Comment