Friday, 20 October 2017

Conte amuonya Jose Mourinho kuwacha kuzungumzia Chelsea

Antonio Conte has snapped back and told Jose Mourinho to stop talking about ChelseaMkufunzi wa Chelsea Antonio Conte anasema kuwa mkufunzi mwenza katika klabu ya Manchester United Jose Mourinho anafaa kujitazama badala ya kuijadili Chelsea
Conte ameonyesha wasiwasi mkubwa kuhusu kikosi chake cha Chelsea kufuatia misururu ya majeraha msimu huu na kusema kuwa sare ya 3-3 dhidi ya Roma katika michuano ya vilabu bingwa imekifanya kikosi chake kuwa katika hali ya dharura.
Mourinho made reference to Conte in his post match comments and irked the Italian
Mourinho ambaye amewahi kuifunza Chelsea mara mbili alinukuliwa akisema kuwa kuna wakufunzi wengine ambao hupenda kulalama sana kuhusu majeraha.
''Kila wakati Mourinho lazima azungumzie kile kinachoendelea Chelsea," alisema Conte
Alipoulizwa kuhusu matamshi ya Mourinho ambayo hayakumlenga Conte moja kwa moja , kocha huyo wa Itali aliongezea: Kila mara , pia msimu uliopita, nadhani ni wakati anafaa kuzungumzia kuhusu kikosi chake na ajitazame badala ya kutazama wenzake.

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...