Saturday, 7 October 2017

Hispania yafuzu kombe la dunia,,Gerard Pique azomewa

Hispania imejihakikishia kushiriki kombe la dunia kwa ushindi mnono dhidi ya Albania 3-0, magoli yaliyofungwa katika nusu ya kwanza ya mchezo huo na Rodrigo (16'), Isco (23') na Thiago (26').
Rodrigo akifunga goli la kwanza

Mabingwa hao wa kombe la dunia 2010 walishinda mechi hiyo dhidi ya Albania na kujiwekea historia ya kushinda mechi 8 kati ya mechi 9 walizocheza kwa kundi G

Hispania ikishangilia goli la pili lililowekwa na Isco
Timu hiyo iliendelea kufurahia mchezo kwa kumiliki mpira vizuri huku wakipata nguvu kutoka kwa mashabiki wao wa nyumbani na kuwaacha Albenia wakiwa katika hali mbaya kimchezo

wachezaji wakishangilia goli la tatu lililotikisa nyavu na thiago
Katika mechi hiyo mchezaji wa Barcelona Gerard Pique aliendelea kuzomewa na mashabiki wa nchi yake richa ya kuonyesha juhudi nzuri katika mchezo huo,, 
Pique mara baada ya kuonyeshwa kadi ya njano
Mchezaji huyo alitoka nje ya uwanja mara baada ya kounyeshwa kadi ya njano, ambayo itamfanya akose mechi dhidi ya israel hapo jumatatu
Mashabiki wakishangilia

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...