Msanii wa muziki Bongo, Aslay ameeleza sababu ya kutoa nyimbo mfululizo.
.
“Tangu nimetoka kwenye band
nimekuwa nikifanya kazi peke yangu natengemea show zangu ziwe na nyimbo zangu tu
siyo za Band ndio maana nafanya kutoa nyimbo nyingi ilimradi hata nikipata show
niwe natumia nyimbo zangu,” amesema Aslay.
“Kingine natoa kazi nyingi kwa
sababu ni nzuri, kazi nzuri ikikaa ndani huwa naogopa kwa sababu naogopa idea
kugongana, kazi nuri ukitoa leo nyingine ukatoa kesho watu watapenda tu” ameongeza.
Kwa mwaka huu Aslay
amefanya vizuri na ngoma kama Mhudumu, Baby, Angekuona, Tete, Pusha, Marioo,
Likizo, Danga na nyinginezo
No comments:
Post a Comment