Wednesday, 18 October 2017

Liverpool kuvunja rekodi, mabingwa watetezi kulazimishwa sare

Mabao 7 ya Liverpool hii leo yavunja rekodi ya Manchester United na kuweka rekodi mpya, matokeo yote haya hapa

Nk Maribor   -      Liverpool
                                                     Roberto Firmono (4',54')
                                                 Phillipe Coutinho (13')
                                                    Mohamed Salah (19' 39')
                                          Chamberlain (86')
                                    Arnold (90+1')
Hii leo ilikuwa mara ya kwanza kwa klabu ya Liverpool kufunga idadi ya mabao 5 katika mechi ya ugenini katika michuano ya Champions League, michezo yao 45 iliyopita ya Champioms League hawakuwahi kufanya hivyo.
Robert Firminho (4), Phellipe Coutinho (13) na Mohamed Salaah (19,40) waliufanya mchezo uende mapumziko huku Liverpool wakiongoza kwa mabao 4 kabla ya Firmninho kuweka la tano kipindi cha pili.
Lakini bao la 6 la Oxlade Chamberlain liliwafanya kuwa klabu ya pili Uingereza kuwahi kufunga mabao 6 katika mchezo wa ugenini ya Champions League rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na Manchester United huku ikiwa timu ya 9 kufanya hivyo.

Na bao la 7 la Alexander Arnold likawafanya Liverpool kuwa timu ya nne kuwahi kufunga jumla ya mabao 7 na zaidi ambapo timu za Bayern Munich, Barcelona na Lyon zimewahi kufanya hivyo na isitoshe kwa usiku wa leo Liverpool ilikuwa timu pekee ambayo haikuruhusu bao.

Manchester City yaendeleza kutoa kipigo

Manchester City waliipiga Napoli bao 2 huku Gabriel Jesus akifunga moja ya bao linalomfanya kufunga mabao 15 ndani ya michezo 22 ikiwa ni mchezo mmoja nyuma ya Kun Aguero wakati anafunga mabao kama hayo alipofika Man City.
Man.City 2  {Raheem Sterling 9', Gabriel Jesus 13' ), (1 Napoli Amadou Diawara 73'( P)}

                       
Mabingwa watetezi wa uefa champions league Real Madrid wametoka sare na Spurs
Real Madrid wakiwa Santiago Bernabeu almanusra waambulie kichapo baada ya bao la kujifunga la Rafael Varane lakini dakika ya 43 ya mchezo Cristiano Ronaldo aliwaokoa Madrid kwa mkwaju wa penati.

REAL MADRID 1    -   1 TOTTENHAM SPURS
 CRISTIANO RONALDO 43' P          RAFAEL VARANE 28' OG
                          
Kwa suluhu ya leo Tottenham Hotspur wanakuwa timu ya tatu kuwahi kupata alama katika uwanja wa Santiago Bernabeu katika michezo ya Madrid 24 iliyopita katika Champions League.


No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...