Iceland imekuwa nchi ndogo zaidi
kuwahi kufuzu kwa Kombe la Dunia baada ya kuwalaza Kosovo 2-0 na
kumaliza kileleni kundi lao la kufuzu kwa michuano hiyo itakayofanyika
Urusi 2018.
Iceland, ambao walifika robofainali Euro 2016, baada ya kuwaondoa England hatua ya 16 bora, ni taifa la raia 335,000 pekee.Ndiyo nchi ya kwanza kufuzu kwa Kombe la Dunia ikiwa na idadi ya watu ambao ni chini ya milioni moja.
Gylfi Sigurdsson wa Everton na Johann Gudmundsson wa Burnley ndio waliofungia taifa hilo Jumatatu.
Sigurdsson aliwapa matumaini kwa kufunga muda mfupi kabla ya mapumziko na kisa akamsaidia Gudmundsson kufunga bao la kuwahakikishia ushindi.
Iceland sasa wameshinda mechi saba kati ya 10 Kundi I la kufuzu kwa Kombe la Dunia.
MATAIFA MADOGO DUNIANI

No comments:
Post a Comment