Sunday, 22 October 2017

yanga yaendeleza kipigo kwa stand united


Nyota wa mchezo huo alikuwa ni Ibrahim Ajib ambaye aliandikia Yanga bao la mapema kupitia mkwaju wa adhabu ndogo dakika ya 24 ambao ulienda moja kwa moja golini. Baadae dakika ya 30 Ajib aliongeza bao la pili na kufanya timu hizo ziende mapumziko Yanga ikiongoza kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili Yanga walirejea na kasi ileile wakiendelea kushambulia lango la Stand United ambapo dakika ya 53 kiungo mpya wa timu hiyo Pius Buswita aliipatia bao la tatu timu yake kabla ya Obrey Chirwa kukamilisha majibu ya Yanga kwa Simba kwa kufunga bao la 4 dakika ya 69.
Baada ya mchezo nahodha wa mabingwa watetezi wa timu hiyo Nadir Haroub amesema matokeo hayo yamewaweka tayari kwaajili ya mchezo wa watani wa jadi jumapili ijayo kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.Yanga sasa inashika nafasi ya pili nyuma ya Simba zote zikiwa na alama 15 zikitofautiana mabao ya kufunga huku Mtibwa Sugar nayo ikiwa kwenye nafasi ya 3 ikiwa na alama 15 sawa na Simba na Yanga ikizidiwa mabao ya kufunga. Mchezo wa wikiendi ijayo ndio utaamua nani aongoze msimamo wa ligi.

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...