Friday, 19 January 2018

Arsenal wenger adaiwa kuitusi klabu ya Borussia

Mkufunzi wa Arsenal Arsene WengerMkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger ''alitukosea heshima'' kwa kuzungumza hadharani kuhusu mchezaji Pierre-Emerick Aubameyang, amesema mkurugenzi wa michezo katika klabu ya Borussia Dortmund Michael Zorc.
Arsenal ina hamu ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Gabon kwa dau la £60m.
Siku ya Alhamisi , Wenger alisema kuwa Aubameyang atafaa sana Arsenal , matamshi ambayo hayakuifurahisha klabu ya Dortmund.
''Tunahisi kwamba ni kukosa heshima kwa Wenger kuzungumzia kuhusu wachezaji wa klabu nyengine'', alisema Zorc.
''Hatujawasiliana na Arsenal''.
''Kwa sasa Arsene Wenger ana maswala mengi yanayompa changamoto ikiwemo mchezo wa wachezaji wake''.
Pierre-Emerick Aubameyang
Aubameyang ameadhibiwa mara mbili kwa utovu wa nidhamu msimu huu.

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...