
Arsenal ina hamu ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Gabon kwa dau la £60m.
Siku ya Alhamisi , Wenger alisema kuwa Aubameyang atafaa sana Arsenal , matamshi ambayo hayakuifurahisha klabu ya Dortmund.
''Tunahisi kwamba ni kukosa heshima kwa Wenger kuzungumzia kuhusu wachezaji wa klabu nyengine'', alisema Zorc.
''Hatujawasiliana na Arsenal''.
''Kwa sasa Arsene Wenger ana maswala mengi yanayompa changamoto ikiwemo mchezo wa wachezaji wake''.


Aubameyang ameadhibiwa mara mbili kwa utovu wa nidhamu msimu huu.
No comments:
Post a Comment