"Naomba niombe radhi kwa Watanzania wote kwa hiki nilichokifanya natambua nimefanya kosa naomba msamaha aweze kunisamehe, pia naomba msamaha kwa mashabiki zangu kwa hiki kilichotokea nimejifunza hivyo nitakuwa Pretty Kind mwingine mpya na kufanya yale yanayotakiwa katika jamii" alisema
Pretty Kind amefungiwa kujihusisha na sanaa kwa takribani miezi sita baada ya kuposti picha katika mtandao wake wa Instagram ikimuonyesha akiwa nusu utupu jambo ambalo ni kinyume na maadili ya Kitanzania na kwenda kinyume na maagizo ya Rais John Pombe Magufuli ambayo aliyatoa hivi karibuni kuwataka wasanii wa kike kuvaa kwa staha.
No comments:
Post a Comment