Sunday, 20 September 2015

waandishi wa habari wapigwa

huwaga nakaa najiuliza hivi sisi watanzania ndio wasahaulifu au vipiii??
lakini sasa kinachonishangaza sasa ni kwamba waandishi wa habari ndio wanaotumiwa na ccm ili kukinadi chama hichi sasa najiuliza ni kwamba hiki chama kinawapa nini?
au ndio waandishi wa habari hawana akili sawa sawa? amabo hawaoni uchungu au hawana lolote sasa wafunguke wakae upande ambao watapata kila kitu 
chadema nyumbani
waandishi wa habari wapigwa  hii ilikuwa ni baada ya makamu wa raisi dr. GARIB BILAL kuwataka polisi kuwalinda waandishi wa habari siku ya alhamisi septemba 2014




Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wakimpa kichapo mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Josephat Isango, nje ya Makao Makuu ya Polisi, Dar es Salaam.

Vurugu zimezuka leo asubuhi katika makao makuu ya jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam nchini Tanzania, muda mfupi baada ya Mwenyekiti taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo – Chadema, Freeman Mbowe, kuwasili kwa ajili ya mahojiano.
Mbowe aliitwa na polisi kwa ajili ya kutoa maelezo kuhusiana na kauli aliyoitoa hivi karibuni ambapo kiongozi huyo alinukuliwa akihamasisha maandamano ya wafuasi wa chama chake kupinga kuendelea kwa vikao vya bunge maalumu la katiba.  Awali vurugu hizo zilihusisha wafuasi wa Chadema na askari wa kutuliza ghasia FFU, lakini ghafla zikabadilika na kuwa kati ya polisi na waandishi wa habari, hatua iliyotokana na polisi kuanza kuwapiga waandishi na kuwafukuza kwa kutumia mbwa maalumu, kitendo ambacho kimelalamikiwa  na  Waandishi  wa  habari.  Tukio la kupigwa kwa waandishi wa habari, limetokea siku moja baada ya Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal, kuvitaka vyombo vya ulinzi na usalama likiwemo jeshi la polisi, kufanya kazi kwa ushirikiano na wanahabari, kutokana na pande zote mbili kuwa na jukumu moja kuu la kuwatumikia Watanzania.   Awali, askari wenye silaha waliwazuia kuingia ndani ya ofisi za makao makuu ya polisi, wabunge kadhaa wa Chadema, akiwemo Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Iramba Mashariki Tundu Lissu, Mbunge wa Ubungo John Mnyika na mwenzake wa jimbo la Ilemela Ezekiah Wenje.
Hatua hiyo ilizusha majibizano baina ya pande hizo ambapo wafuasi wa Chadema walikuwa waking'ang'ania wabunge wao waingie ndani kwa madai kuwa baadhi ya wabunge hao wana nyadhifa muhimu ndani ya chama na kwamba ingekuwa vema waingie na kufahamu anachohojiwa Mwenyekiti wao.

baba wa watu mwandishi wa habari analia kwa uchungu kwa kile kilichotokea hapo 


No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...