Rwanda 1-2 Tanzania: anasema Hamisi, Simon Msuva ameipeleka Kilimanjaro Stars kwenda robo fainali
mashabiki wa Kilimanjaro Stars wakiishangilia timu yao katika mechi yao. timu ya kilimanjaro stars ya tanzania imefanikiwa kuingia robo fainali baada ya kuilaza timu ya taifa ya rwanda kwa goli 2 kwa 1 katika uwanja wa Hawassa Stadium
mchezaji hatari wa Rwanda Jacques Tuyisenge aliwapatia rwanda goli kwenye dakika ya 86, lakini walikuwa wamechelewa.
Katika mechi hiyo iliyopigwa mjini Wassa, Stars ilipata bao moja katika kila kipindi.
Bao la kwanza lilifungwa na Said Ndemla na la pili likatupiwa na Simon Msuva katika kipindi cha pili baada ya kipa wa Rwanda kufanya uzembe.
Stars imefikisha ponti sita baada ya kuifunga Somalia kwa mabao 4-0 katika mechi ya kwanza.
Tayari ina nafasi ya kufuzu, kwani hata timu nyingine katika kundi lake itafikisha pointi 6, bado itakuwa na nafasi, zikifikisha timu mbili, bado itakuwa na nafasi ya best looser.
Mechi ya mwisho ya Kili Stars hatua ya makundi itakuwa dhidi ya wenyeji Ethiopia walioanza michuano kwa kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Rwanda.
Katika mechi ya awali, Zanzibar Heroes iliandikwa mabao 4-0 Uganda ambao walianza michuano hiyo kwa kupoteza kwa mabao 2-0 dhidi ya Kenya.
No comments:
Post a Comment