Sunday, 15 November 2015

RAISI WA TANZANIA DK JOHN POMBE MAGUFULI AWAFURAHISHA WAKAZI WA MOROGORO

Yusufu Jumanne Mkazi wa Kihonda alisema kwamba  kiongozi huyo  anaonesha  kwamba   ana uwezo mkubwa katika kuongoza taifa  kutokana na namna alivyoweza kufanya ziara ya kushtukiza katika ofisi mbalimbali baada kuapishwa.
Amesema kwa hatua hiyo ameweza kufufua matumaini  kwa wananchi na kuweza kufanya watumishi wa umma kuwa wachapakazi  kutokana na kauli mbiu ya hapa kazi tu.
Naye Emmanueli Victor ambaye ni mwanafunzi katika shule ya msingi Sua  amemwomba raisi  Magufuli kuweza kuwapa kipaumbele wanafunzi wa shule  za msingi kwa  kuwalipa walimu madai yao sambamba na kuongeza mishahara ya walimu kwani kufanya hivyo kutawezesha wanafunzi wapate elimu bora
Pia Abou Chongole mkazi wa Magadu  alimwomba  mheshimiwa  Raisi  kuweza kutatua matatizo mbalimbali katika mkoa wa morogoro hususani tatizo la  mgogoro wa wakulima  na wafugaji wilayani  kilosa  kwani tatizo hili limekuwa sugu kutokana  na awamu iliyopita kutotatua tatizo hilo.

No comments:

Featured Post

Ronaldo kaonyesha yeye ni mwamba dhidi ya Salah

Mchezaji  wa klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Ureno amefunga magoli mawili  (2) katika mechi kati ya Ureno na Misri...